Jumamosi, 26 Julai 2014
sudan kusini yakabiliwa na njaa
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni 600 kutoa fedha hizo.
PEPE REINA : NITAGOMBANIA NAMBA
Mlinda mlango wa klabu ya Liverpool Pepe Reina 31, amedai kuwa yupo tayari kubaki katika klabu hiyo mara baada ya kumaliza msimu wa 2014/2015 akicheza kwa mkopo klabu ya Napoli.
Mke wa Mbunge Amuua Beki tatu
Mfanyakazi wa ndani wa Mbunge wa Jimbo la Moshi vijijini Cyril Chami (CCM) aitwaye Mariam Said (16) amefariki dunia mapema alfajiri ya leo ikiaminika kwamba kifo chake kimesababishwa na kipigo toka kwa mke wa Mbunge huyo.
DRAKE : J COLE & I AM THE KING OF RAP
Rapper kutoka kundi la Young Money Drake anasema Yeye na J Cole ndio Wafalme wa muziki wa Rap Marekani. Drake amesema haya baada ya kufanya show na Rapper J Coleambayo pia rapper Kendrick Lamar alikuwepo kwenye ziara hio ya “Dollar & A Dream”
Van Gaal akutana na Fergie
Louis van Gaal atakaa kitako na Sir Alex Ferguson kwa mara ya kwanza mwishoni mwa juma wakati kocha huyo wa zamani wa Manchester United atakapojiunga na timu hiyo mjini Washington.
Nakumatt kuingia Mlimani City
Wauzaji wa reja reja wa kanda na wamiliki wa Nakumatt, watafungua milango ya tawi lao rasmi kesho Jumapili asubuhi lililopo katika duka kubwa la Mlimani City katika wilaya ya Kinondoni.
Tawi hilo jipya, litajulikana kama “Nakumatt Mlimani” litatoa huduma zenye manufaa kwa wateja wake wa jiji la Dar es Salaam.
Ufunguzi wa duka hilo utahudhuriwa na Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Mheshimiwa Janet Mbene.
