SERIKALI imeahidi kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wa ziara ya magwiji wa Real Madrid maarufu kama ‘Real Madrid Legends’ wanaotarajia kutua nchini Agosti 22 mwaka huu na kucheza mechi moja ya kirafiki dhidi ya kikosi maalumu cha nyota wa Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa habari, vijana, utamaduni na michezo, Dkt. Fenella Mukangara alipotembelewa na kamati ya maandalizi ya ziara hiyo katika ofisi yake katikati ya jiji la Dar es salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni