Sports and Entertainment

Alhamisi, 29 Januari 2015

Obama azua gumzo Saud Arabia

Hakuna maoni :

Michelle Obama wakati wa Ziara ya Rais Obama Saudi Arabia 
 
Mkewe Rais wa Marekani Barack Obama, Michelle Obama alipowasili nchini Saudi Arabia na mumewe bila ya kujitanda kichwa chake kwa kitambaa, wengi walitarajia kwamba mitandao ya kijamii nchini humo ingewaka moto kwa mingon'ono.

Lakini mambo yalikuwa tofauti maana kimya kilikuwa kikuu. 

Ingawa vyombo kadhaa vya habari Ulaya, viliripoti kuhusu utata mkubwa kutokea kwenye mitandao ya kijamii, alama ya njia ya reli kwenye mtandao wa Twitter kwa lugha ya kiarabu...ikimaanisha ....''Michelle Obama bila mtandio''...ujumbe huo ilisambazwa kwenye mtandao huo zaidi ya mara 2,5000.

Hii sio idadi kubwa ya watu waliousambaza ujumbe huo lakini pia sio ndogo sana katika nchi yenye watumiaji wengi wa Twitter.

Pia inaarifiwa ujumbe huo ulizidiwa nguvu na ujumbe mwingine uliotumwa kwenye Twitter dhidi ya ziara ya Rais Obama nkatika ufalme huo.

''Mfalme Salman amwacha Obama na kwenda kuomba,'' huu ndio ulikuwa ujumbe mwingine uliosambazwa sana kwenye Twitter kuhusu ziara ya Obama nchini humo.
Ujumbe huo: "Mfalme Salman amwacha Obama na kwenda kuomba,'' uliwavutia zaidi ya watu 170,000.
Kuna baadhi ya viongozi waliowahi kwnda Saudia bila ya kufunika vichwa vyao
Wananchi katika ufalme huo walisambaza ujumbe huo kama njia yao ya kuonyesha wlaivyofurahishwa na mfalme mpya, Salman kumwacha Obama na kwenda kusali,kama ilivyoonekana kwenye video iliyowekwa kwenye Youtube.

''Huyu ndiye mwanamume aliyemwacha kiongozi wa nchi muhimu zaidi duniani akimsubiri wakati akienda kusali'', aliandika mtu mmoja kwenye mtandao wa Twitter.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni