Sports and Entertainment

Ijumaa, 1 Agosti 2014

EBOLA YAZIDI KUTIKISA, WATU 57 ZAIDI WAFARIKI

Hakuna maoni :
Israel imesema haitaondoa majeshi  yake kutoka Gaza hadi pale itakapomaliza  kazi ya kuharibu mfumo  wa  njia za chini ya ardhi , licha  ya  shutuma  kazi kutoka Umoja wa  Mataifa  kuhusiana  na idadi  ya  vifo  vya raia  wa Kipalestina. Akizungumza katika  mkutano maalum  wa baraza  la  mawaziri  mjini  Tel Aviv, waziri  mkuu  Benjamin Netanyahu  amesema  hatakubali  hatua  yoyote  ya kusitisha  mapigano  ambayo  haitaruhusu  majeshi  yake kuendelea  kuharibu  mfumo  wa  mahandaki  hayo  ya wapiganaji  yanayotumiwa  kushambulia  ardhi  ya  Israel.
Wakati  huo  huo  baraza  la  Usalama  la  Umoja  wa Mataifa  limefanya  kikao  cha  dharura   kuhusu  Gaza baada  ya  shambulio  dhidi  ya  shule   katika  ukanda  wa Gaza. Mkuu  wa  idara  ya  misaada  ya  dharura  ya Umoja  wa  mataifa  Valerie Amos  amesema  kuwa  pande zote  mbili  Israel  na  Hamas  zinapaswa  kuangalia  sheria na  kanuni  za  mapigano.
Ametaka  pande  hizo  kuchukua  hatua  ya kusitisha mapigano  kwa  muda ili  kutoa  misaada  kwa  watu wanaohitaji  misaada  hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni