Alhamisi, 18 Septemba 2014
Messi achekelea miaka 14 ya uwepo wake Barcelona
Ni miaka 14 tangu Lionel Messi ajiunge Barcelona – wakati uliofanya awe mchezaji hodari aliyewahi kuonekana.

Lionel Messi alituma picha hii kwenye ukarasa wake wa Facebook kusherehekea miaka 14 akiwa mchezaji wa Barcelona.
Mchawi huyo wa Argentina amekuwa mchezaji wa Catalans, ambao wana mengi ya kumlipa nyota huyo, 27 kutokana na mafanikio yao.
Akisherehekea kipindi hiko, wote Lionel Messi na klabu walituma kumbukumbu ya usajili wake kutoka miaka yote iliyopita.
Messi alisema kwenye Facebook: “Septemba 17, 2000, niliwasili Barcelona FC. Leo (jana) ni mwaka wa 14 kwenye klabu.”
“Ningependa kusema asante kwa wachezaji wenzangu wote, makocha, mashabiki, viongozi wa bodi na wafanyakazi ambao nimekuwa na furaha kufanya nao kazi na msaada ambao wamekuwa wakinipa. Kumbatio (Hugs)”.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni