Sports and Entertainment

Jumamosi, 6 Desemba 2014

Chris Brown nae achepuka kwenye "Project"

Hakuna maoni :
chris-brown-and-karruecheUjumbe alioandika mchumba wa mwanamuziki Chris Brown, Karruece kwenye ukurasa wake wa Twitter huenda ukawa haujawashtua  mashabiki wao hasa kutokana na wawili hao kuzoeleka kuwa katika mapenzi ya kuachana na kurudiana mara kwa mara.
”Looks like I’m a single lady again” aliandika Karruece akimaanisha kwa sasa amerudi tena sokoni.
Ujumbe wa mwanadada huyo unakuja kufuatia siku za hivi karibuni Chris Brown kunaswa na kamera za mapaparazi akiwatongoza warembo wawili nje ya klabu moja ya usiku sambamba na ushahidi wa picha uliodai kuwa alivunja nao amri ya sita.
Mpaka sasa Sio Chris Brown wala Karruece aliyetangaza rasmi kuvunjika kwa penzi lao.
Wacha Muvi iendelee, huenda labda nao walikuwa kwenye Projekti.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni